Feb 2, 2009

MJINI KUMEWAKA MOTO,SIJUI MADUKA YATAFUNGWA?????NA MAGARI YATAUZWA AU ?????????????NIKIZAAAAAAAZAAAAAAAAAAAAAA


Nikizaza kikubwa kama sio kasheshe kwa wapenda bure wa mjini na wale warembo wasiojithamini...............
Yule mfadhili mkubwa wa warembo sasa yuko mashakani,kwake yeye sio tatizo sana kuwa mashakani,ila mashaka wanayo watu waliokuwa wanafadhiliwa maana ni aibu ya mwaka,wale waliopewa magari mekundu wengi waliyabadili rangi sasa wanaumiza kichwa kwa mafuta,waliofunguliwa maduka wanawaza watayafunga lini kama si kupaka hizo cream wakajimaliza kama sio kujikoboa,sababu kama kujichubua walujichubua mpaka wakabaki sugu sasa watakunywa mikorogo hahaha.
Tisa kumi wanaume wamjini wao imekuwa kinyume,wamefurahi maana huyo mfadhili aliwachukulia sana wanawake zao hahhaha,wanatamani wamuombee aongezewe miaka hata iwe milele,japo kuwa hapo naunga mikono sio mkono hahaha.
Najiuliza sasa kama maduka yatafungwa na magari yatauzwa au kuyapaki,je dawa za ile kitu watapata wapi????????????????????//maana mkubwa alikuwa anakupa hela ya doziiiii.Nikajiuliza tena je fadhila zile alizowapa si ndio wakati wakulipa fadhila haya sasa,uzeni magari mnunue dawa,wenye maduka pangisheni,mlioolewa sasa sijui mtatoka kwenye ndoa muuze nyumba..............................mmh inatisha sana huo ni mwanzo tuu msishutuke maana wengine matumbo yanawauma....bado yeye mkubwa kuanza kuumwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa...............................hii inaitwa ni bakora ya mwalimu wa zamuuuuuuuuuuuuuuuuu

Jan 22, 2009

MASAKI NA MBAGALA WAPI BORA?????????????????????

Swali hili wamekuwa wakiulizana watu mbali mbali, na wengine kutuambiana kuwa, wao wanaokaa masaki ni watoto wa geti kali na wahali ya juu kwa ujumla mambo safi,wakati wanaokaa mbagala wanaitwa kuku wa kienyeji yaani wasiofugika au watoto wa uswahilini.
Kama kawaida ya kwa nafasi huwa tunaweka vitu bayana,haswa vile vya ukweli.kwa upande wangu kwa kuwaangalia tuu hivi kwa machoni siwezi kujua yupi anatokea mbagala na yupi anatokea Masaki,pasipo kuambiwa na mtu kuwa huyu ni wamasaki na huyu ni mbagala...nikasema nisikilize wenyewe wakazi wa maeneo hayo.Nilibahatika kuanza kukutana na watu wa masaki na haya yalikuwa ndio majibu yao,Nani asiejua kuwa watu wa masaki ndio wanaongoza kwa kuwa na hela,,,,mmh hapo nikajijibu kwenye nafsi yangu watu wa mbagala kwahiyo hawana hela?....mmh nikasema sasa wanatumia nini?pili watu wamasaki wengi tunaendesha magari,,.....mmmmh haya lakini moyoni tuu najijibu,tatu Nyumba zetu ni nzuri na safi,......hapo kidogo kuna ukweli lakini kwenye usafi....nne kuna maghorofa mengi.....hee nikasema sio ya serikali lakini....tano Hakuna wakabaji huku wala wabakaji.......mmh nikasema watoke wapi wakati kuna nyumba za wakubwa wa nchi nyingi,,,,,,.....Sita umeme huwa haukatiki ovyo......hii kweli,,,,sababu hakuuzwi bangi huku zaidi ya bia na sigara...............sasa kwahiyo mbagala hakuuzwi bia,wanauza nini gongo?,,,mweeeeh....nikasema hayo nimeyaskia sasa wambagala wao wanasemaje?
Skia ndugu mwandishi,kwanza nikufahamishe uku mbagala nyumba ni zakwetu wenyewe hakuna ya buree huku,wala ya kulipa mwisho wamwezi laki mmoja mpaka umalize deni ndio nyumba iwe yako........nikasema heee mboni wanapiga kwenyewe.....kuhusu usafi je unasemaje,,,,,,bwana weee nyumba ni zakwetu wenyewe sasa usafi huo wanaoutaka wao ni upi wakupaka rangi nyumba au?nikasema watu wa huku wanaongea sana mmmh.....je kuhusu kuwa na magari?mmh hawaoni huku pia kunafoleni kwenda mjini nakurudi kama hakuna magari foleni ya nini?nikasema kazi kweli kweli....vipi kuhusu umeme kukatika ovyo uku kwenu,,,,sie hilo si tatizo kwetu sababu tunatumia sana umeme wa asili....hapo kidogo nikaogopa,,..je wakabaji na wabakajii,....weeeeeeeeeee uku hamna vya hivyo kila unaemuona anasilaha yake nani atamsogelea alafu uku tunajuana.....mmmhkazi kweli kweli....
Kwa kuwasikiliza watu hawa,nimeona jibu ni mmoja tu kila mtu anapenda kwake na kusifia kwake,na kwa majibu yao,yameniweka njia panda mpaka mimi sijui wewe msomajii wa habari hii,mi naona ni drooooooooooooooooooo au wenzangu mnaonaje? comment kwa chini hapo

MAISHA MAFUPI YENYE STAREHE YAMEMALIZA WENGI MJINI

Wenye mji wenyewe wanausemi wao siku hizi,bora waishi maisha mafupi yenye starehe kuliko marefu yenye shida...........................
Kwa mwendo huu atapona mtu kweli?mpaka kufikia hapo ujue watu wameamua tayari kujilipua kama si kujitoa muhanga ,yani lolote na liwe bora mambo yangu yawe safi.sijui hawajiulizi yawe safi kwa muda gani maana wanafikiri miaka kumi mbele pasipo fahamu inaweza ikawa mwaka na nusu......haaaaaaaaaaaaaaaaa.
Imekuwa ni kama tabia jijini kwa wasichana na wavulana,kufata mtu kwa ajili ya mfukoni mwake kukoje,haijalishi uyo mtu afya yake ikoje? wao bora chapaa au pesa tuu,ukimuuliza unamjua? ooh utajibiwa nimjue kwani ndugu yangu na kwamba wao wanaangalia pesa na usafiri.Jiulize sasa yale matangazo yote ya ukimwi watu hawayaoni?au wanaona ni matangazo ya pipi kifua?
Inasikitisha sana kuona watu wanadanganyika kwa usafiri na pesa,na kupelekea kutojali afya zao,sasa huu ugonjwa wa ukimwi kwa mwendo huu,utaisha kweli?Ukiwaona mjini wanatembelea magari mazuri, wenyewe wanasema wanatesa,jiulize kutesa uko kwa muda mfupi kwa nini?maana mwaka bararani miaka miwili kitandani.......Ndio wameamua sasa maisha mafupi yenye starehe...........Ila mnaowatesa ni wachache na mtawaacha kwa tamaa zenu za maisha ya juu.

WAREMBO NA KAMATI YA WAGENI.....WAPI NA WAPI???????????????


Ama kweli wazazi wana sababu ya kuwakatilia watoto wao kutoshiriki katiko mashindano yoyote ya urembo Tanzania.
Hapo mwanzo nilikuwa mmoja ya watu niliyekuwa nikiwalaumu wazazi kwanini wanawanyima uhuru watoto wao,na pia kuwaomba watoe dhana potofu kuwa urembo ni uhuni.Lakini kutokana na mambo wanayofanya walimbwende hawa hivi sasa,inanifanya niunge mkono dhana ya wazazi kuwa urembo na uhuni vipo sambamba.
Hapa ninapoandika habari hii,nina masikitiko na mshutuko mkubwa kwa yale niliyoyaskia na kuyaona yanatendeka jijini dar na warembo hawa,baada ya kufanya shughuli za jamii, na kuijenga jamii kuelewa kuwa urembo ni kazi kama kazi nyingine,wao ndo kwanza wanaionyesha jamii kuwa urembo ni uhuni.Huwezi amini ndugu msomaji wa kwa nafasi kuwa WALIMBWENDE wa bongo hivi sasa wamepewa idara ya kukaribisha wageni,,,,,,,,,,,,,,,,,,usidhani wanawaonyesha vitega uchumi vya nchi yetu???????maana hapo wangekuwa wanalisaidia taifa letu kwa njia mmoja au nyingine....
Kwa wale wasiojua na wasio na taarifa,ni hivi siku hizi akija mgeni yoyote wa kutoka nje ya nchi yetu, haswa wale maarufu kama,wachezaji,wanamuziki na wengineo,basi warembo huitwa sehemu maalum wakachill kama wenyewe wana vyoita.....sasa hapo mwenye bahati yake haya atapata,asie na bahati ndio basi tena,,,,,,,,,,,,,,,,,,sasa hii si ni aibu jamani....sasa hapa ndipo ninapokosa maana halisi ya urembo wa bongo unavyotumika......yani kukaribisha wageni,,,mmh na kuchillllllllllll naooo.....haaaaaaaaaaaaa.....KAMATI HUSIKA LENU HILO TUNAWAKILISHA..........na ndio maana wengine wanakutwa katika mahoteli makubwa wamekunja nne na kinywaji kimoja masaa matatu .nyie walimbwende vipiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.?

Jan 21, 2009

oooh.VALENTINE DAY BONGO NI FUMANIZI DAY......

Valentine day inajulikana dunia nzima kuwa ni siku ya wapendanao,lakini kwa wabongo mambo huwa tofauti kwao ni fumanizi dayyyyyyyyyyyyyy.
Wengi wenu mtakuwa mmesema hivi huyu au hawa watu wa kwa nafasi inakuwaje wanaongea ukweli mtupu na wanazipata wapi hizi,jibu ni kwamba kuwasoma wabongo auhitaji darasa wala ramani kwa jinsi vitu vyao visivyo jificha.
Leo naizungumzia hii siku ya tarehe 14 mwezi wa pili kuwa ni siku ya kupumzika kama si kumtoa mwenzi wako, au familia yako, mkawa na furaha na amani bila maudhi ya hapa na pale, yasiyo na kichwa wala miguu.Kuna wabongo wengine wale ambao wanamahusiano na zaidi ya mmoja ,wao siku hii huwa tofauti kwao,baada ya kuwa siku ya furaha kwao karaha na mpaka inafikia kuichukia hii siku,maana anajua za mwizi zimefika na hajui ajigawe vipi na kila mtu siku hiyo anataka kuwa na mtuye,,,,,hapo ndipo kwenye patashika nguo kuchanika na sababu tele..
Natumia wakati huo kuwajulisha baadhi ya sababu zinazotumika kwa siku hii,MOJA....Mpenzi huanza kununa siku saba kama si kumi kabla,bila sababu ya maana.PILI............kutafuta ugonjwa asio kuwa nao ukiongea nae kwenye simu au kuonana nae,,,,,.TATU......Utamsikia tarehe kumi na nne nitakuwa na familia yangu leo baba au mama kanipigia kunijulisha......NNE....Unaweza usionane nae kwa muda wa wiki mbili kabla kwa kudai kuwa yuko busy.....na TANO....Huamua kuzima simu kabisa.Ukiona mwenza wako anadalili mmoja wapo kati ya hizo ujue kwa hapo huna mwenza ni tapeli wa mapenzi tuu,na kujiepusha na ugomvi na fumanizi,usimfatilie wala usiende kwake bila ahadi kwa maana siku hii ni siku ya ngumi za wazi wazi hapa jijini..........na ukimkuta sehemu na wewe jifanye haumjui japo kuwa ni nguuumu.
Cha kujiuliza ni kwanini wabongo sio waaminifu wamapenzi jamani?????????na kwanini asilimia kubwa ya mtu na mwenzie wanakuwa na makovu kama si usoni,mwilini ukimuuliza kulikoni nilipigwa na mupenziiii wanguuu,,,,,,,,,,,, haaaaaaaaaaa.......mupenzi gani huyu huyu au mpenzi jini.......Najua wengine nimewaharibia ila ni zama za ukweli na uwazi mwambie unae wako valentine day wako na sio usubiri fumanizi daya wakoooo,

USHOGA TANZANIA NI HALALI???????????????????????????

Leo tumeingia kwenye mada kubwa kidogo na ambayo iko tofauti sana na mila na desturi zetu, dini zinakataza pia.
Si kitu kipya sana katika jamii yetu kwa hivi sasa ila kwa zamani kilikuwa ni kitu tofauti kabisa,na si kingine ila ni USHOGA.Inaeleweka kabisa si katika jamii tuu,ila pia katika dinia zote iwe ya kikristo au kiislam hata wapagani mambo haya yanapingwa vikali.
Inasikitisha kuona vitendo hivi sasa vimekuwa vinafanyika hadharani,bila aibu au staha jambo ambalo linasikitisha sana,na kupelekea kujiuliza tunaelekea wapi watanzania?Kama si mwisho wa dunia au mwisho wa IMANI NA AMANI?
Vitendo hivi zamani vilikuwa vinajulikana kuwa vinafanyika tanzania visiwani yaani Zanzibar,Tanga na Mombasa,lakini hali ya sasa hivi ni tofauti kabisa na kupelekea uchafuu huo kuhamia tanzania bara haswa jiji dar.Kama utakuwa mtokaji wa sehemu za starehe utaungana mkono na mimi kuwa vimekithiri kabisa,si sehemu za TAARABU na sehemu za MUZIKI WA DANSI,cha ajabu ni kwamba watu wanawafurahia na kukaa nao pamoja kabisa,na ukiangalia watu wao wakaribu ni VIOO VYA JAMII,nadhani kila mtu anaelewa maana ya kioo cha jamii.sasa watu hawa walitakiwa wawe mfano wa kuigwa kwa kuwatenga hawa watu lakini matokeo yake wanakaa nao na kucheka nao na wengine mpaka kuwaweka katika matangazo yao ya vipindi......................Baadhi ya watu wamesema kuwa watu maarufu wanawake wanaongozana nao ili waweza kupata mabuziiiiiii,,,,mmh eti kwa kuwa hawa mashoga ni makuwadii wakubwa..hapo kidogo nikaelewa ni kwa nini wasichana wengi wa mjini wanapenda kutoka nao kumbe wanawatafutia mabuziiiiiiiiiiiiiii,,......eeh nilichoka.Nikauliza na Wanaume pia mbona waongozana nao nilivyojibiwa ndipo nilipochooka kabisaaa....na kufanya nijiulize ushoga Tanzania unaelekea kwenye uhalali??????????????????????????????????Kama nguo za kike wanavaa na kusifiwa kuwa wamependeza,wanaenda mpaka kwenye kitchen party,wanatangaza matangazo pia, kinachoacha maswali mengi kichwani mwangu ni kwamba hivi wanawafurahia kwasababu hiki ni kitu cha kawaida kabisa, je na wao wanafanya vitendo hivi au? kipi kilichobaki?????????na wapi tunaelekea WATANZANIA WENZANGUUU..........................................................?

Jan 20, 2009

WATOTO WANAHAM NAE ........MWEEEEEEEEEEEEEEEEEEH


Tangazo jamani,kwa wote wenye mawasiliano na kijana huyu na wanaepajua wapi anapatikana,ili tuwasaidie watoto wetu ambao ni taifa la kesho.
Kijana huyu anajulikana sana kwa kuwaburudisha watoto na watoto pia huwa wanampenda sana mpaka kumtafuta na kuwa na hamu ya kumsikia kijana huyu.Sio mwingine ni MR NICE au mzee wa kidali poo kama anavyojulikana na wengi.
Mwanamziki huyu ambae alikuja na staili yake ya takeu na kuimba nyimbo nyingi za watoto na ambazo zilikuwa zinachezeka sana na yeye mwenyewe akiwa mchezaji mkubwa sijui amefia wapi kama sio kufichwa.Nimekaa nikajiuliza kuwa vipi mbona haimbi tena,jibu la kwanza likawa au anamuogopa ZE DUDU BAYA?AU KIKOSI CHA MIZINGA?Nikasema hapana kwa kuwa wapo watu wakumlinda yaani,polisi kama si wanajeshi.Jibu la pili likawa ooooooooooh NYIMBO ZOTE ZA WATOTO KAZIMALIZA haaahhahahahhaah,nikasema kuna ukweli hapo.
Natumia nafasi hii kumbusha kuwa upo wimbo wa watoto mmoja kausahau nao ni KICHURA CHURA mmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmh,......Haya nenda studio NICE wimbo huo....teheeeeeeeeeeee

KILEVI AU ?,UGORO,PARIKI,KUBERI .......................

Kumekuwa na mtindo sijui niite au kuigana tuu au kufata mkumbo,kwa hivi sasa kwa baadhi ya vijana mpaka wale wanaitwa kioo cha jamii pia kutumia.
Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la watumiaji wa ugoro,pariki na kuberi kwa vijana wa sasa.inashindwa kueleweka kipi kinachowapelekea kutumia ulevyi huu kama ni ulevyi kweli.
Hapo zamani ni Wazee tuu ndio waliokuwa wantumia sana ugoro,pamoja na sigara.lakini hivi sasa ni vijana kwa wazee ndo wanatumia ulevyi huo na pia hao wazee pia wamepunguza kama sio kuacha kabisa.Kilichopelekea kuandika habari hii katika kwa nafasi ni masikitiko yangu kwa hawa vijana wanaona hivi sasa ujana unaraha na majiayamoto.mi naamini hakuna kilevyi kisichokuwa na madhara.ukiachana na meno yao kuharibika na kutia kinyaa kwa ugorona mapariki naamini kuna madhara ya ndani kwa ndani.
Wao wenyewe wanakwambia vinawachangamsha.sasa sijui ni kwa kutema mate au sana na kuchafua jiji?au kwa vinywa vyao kuwa vichafu?
Uchunguzi uliofanywa na safu hii ,umegundua kuwa ulevi huo unatumiwa sna na vijana hawa ni kwa sababu ya unafuu wake na pia,hawaombwi pafu au kogongea kama wenyewe wanavyosema.............lakini tunawakumbusha kuwa jamani starehe gharamaaaa....na mnakera watu wengi mnavyotema mate ovyo ovyo kama wajawazito?au kuna mimba za kime.......aibuuu hiiiiiiiiiiiiiiii

CHAKULA BORA JIJINI DAR

Jijini dar au bongo kama inavyojulikana na wengi,kwa hivi sasa watu wanapewa buree chakula ni raha tupu kama si karaha.
Watu wa jijini mwa kandoro,wamebahatika kupata nafasi ya pekee ya kupata chakula bure bila kulipia hata shilingi mmoja.baadhi ya watu wanaweza wakasema wanabahati na wanapendelewa bora na wao waende jijini.lakini siku zote huwa vyabure vinamazara jamani,wala msipoteze nauli zenu kukimblia bureee hiyo.
Najua wengi wenu mtataka kujua ni chakula gani watu wa bongo wnapewa bure ,utakuwa unajiuliza ni MAHARAGE?UBWABWA?UGALI?AU MAKANDE?hahahha maana ndio kinapendwa na wengi.hapana wenzenu wanapata chakula ambacho kinamadhara baadae,je unajua ni kipi?Usione wala kudhani wanabahati ukalalamika kuwa JK mbona kwasahau na nyie.
kiukweli na kwa ufahamu wangu mdogo.wakazi hawa wanapata chakula cha vumbiiiiiiiiiiiii tuu kutokana na utengenezwaji wa barara usio isha.tunajua ukifika msimu wa maembe huwa kunakuwa na kipindupindu kwa wingi watu wanakuwa wanaurafiki na choo,lakini kwa kula vumbi watapata choo cha smenti kama si zege.poleeeni sana sasa ni wakati wa vijini kula raha.

Jan 19, 2009

YUPO WAPIIIII HUYU MWANAMZIKI????????????????

Kutokana na mapenzi niliyokuwa nayo kwa mwanamzkiii huyo na alivyokuwa anapendwa na washabiki wengi haina budi kuuliza yuko wapii?
Ni yule yule DOCTOR MUUMINI ni yule kijana hodari kocha wa dunia.......hahaha hiyo ni sehemu tuu ya nyimbo ya mwanamuziki huyo,ambaye alitingisha tanzania nzima kwa sauti yake nzuri,lakini hivi sasa sijui yuko kwa wapi kwa maana mmh,ndo maana wahenga walisema ngoma ikivuma sana mwisho wake hupasuka.huyu kijana alikuwa ni mtunzi mzuri na muimbaji mzuri wote tunalikubali.
Nikiwa kama mshabiki wa nyimbo zake na huwa nazisikiliza mpaka leo hii,huwa sichoki kusema kipaji anachooo ooh nimekumbuka alikuwa nacho sababu sijui sasa hivi kipo wapi au amekimbia wazaire hhahaha.Mpaka hivi sasa huwa sichoki kusikiliza TUNDA SPECIAL,MGUMBA,na nyinginezo.
Ombi langu linaenda kwa wamiliki wa bendi na maproducer jamani,muoneeni huruma mtaanzania mwenzenu kama aliwakosea,ni mtoto kukosa ni kawaida msameheni na mumrudishe studio,,,,,hahahaha...............Na wewe kaka MUUMINI acha ujuaji wakati sauti bila bendi ni sawa na kasuku anasauti nzuri lakini wimbo wake haunogiiiiiiiiiiiiiiiiiiii............peke yako huwezi kutokaaa au bora uanze kuimba bongo freva.....sipati picha maana nako kugumu mnooo

HEHEHEEE ETI WANAJIITA WANAUME WA MJINI

Eti mimi ni mwanaume wa mjini ooh unachezea bahati mmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmm.Kama bahati ni hiyo basi jua kuwa bahati duniani zimeishaaaaaa.
Kumekuwa na baadhi ya wavulana wamjini kama wanavyojiita wao wenyewe kujisifia sana kuwa wao ndio wenye mji wa dar,sasa waulize wanakitu gani cha kuonyesha wao ni wamjini na utamtambuaje kuwa huyu ni wamjini?hapo ndipo utakapocheka mpaka basi.Eti anajulikana mjini kwa kuvaa vizuri hahahahha,na pili ANAUWEZO WA KUTEMBEA NA MSICHANA YOYOTE MAARUFU hehehe,Tatu ANATAJWA KWENYE NYIMBO,Ohooooooooo,na nne ANAMILIKI GARI,Hapo sasa wakati nyumba kapanga.
Sasa najiuliza hizo sifa mbona hazifanyi uwe mtu wa mjini kama wao wanavyojiita au hawajielewi.Au wanadhani jamii yote haina upeo kama wao?yani mtu utembelee gari zuri uku unalaa miguu nje au unaoga kwa foleni ni akili au matope?mie nilijua mambo hayo wanafanya wakongo tuu maana wao kuvaa na kujikoroga ndo kazi yao hata walale chini.Chakushangaza mambo hayo hawa wanaume wa mjini wameyapatia wapi?Na alie waambia kuwa na wasichana wengi ndio ujanja ni nani?
Ukweli ni kwamba huo ni ushamba tuu kaka zangu,siku hizi watu wanaangalia maendeleo sio sifa zenu za kitoto,kuvaa cheni kubwa hata kama la kuchovya,kubeba simu ya gharama hata kama ya wizi pale azam,Kuendesha gari zuri hata kama lakuazima,Au kuwa na wasichana wengi,kifupi ni kwamba tunajua yupi ni mwanaume wa mjini na yupi sie, kwa kuangalia MAENDELEOOOOOOOOOOOOO...........................Kuvaa hata watoto wanavaa si tuna wanunuliwa na wazazi wao.hahahahahahah.....

MITINDO MINGINE ACHA IKUPITEEEEEEEEEEEEEEEEEE SHOSTITO


Mtu akikupenda na akikujali ndio atakae kuambia ukweli hata ukikuuma au laah,lakini akikuacha bora liende ujue hana mapenzi na wewe.
Kilichopelekea kuandika habari hii ni baadhi ya tabia ya watu kutoangalia kipi kinawafaa kutokana na miili yao,wao huvaa tuu bora kitu kipo kwenye chati hata kama ni kituko kwao.
Hivi sasa kila msichana utakaemuona mjini anataka kuonyesha kiuno chake,hata kama kiuno kipo juu kama kamba au hana kiuno au ana wowowo kuubwa sana.kiufupi huu mtindo wa kuvalia nguo chini ya kiuno haujawekwa kwa wote jamani,kizungu wanaita low cut,ni kwa ajili ya wale wasio na nyama za mgongo,waliokatika kiunoni na wasio na wowowo kabisa.hii inakera sana unapotembea mjini unamuona mwanamke mwenzio kaachia vitu nje huku baadhi ya vijana wakimcheka na mwisho wa siku unajiona hata wewe usievaa hivyo unapata aibu kwa niaba yake.
Kwa kumuangalia tu mtu wa aina hiyo,huwa unajiuliza hivi huko nyumbani kwake anakaa peke yake?au ana msichana wakazi ambaye anamuogopa boss wake kumueleza ukweli na kubaki anamchekea tumboni?au kioo chake kinamuonyesha sura tuu?
Ndipo hapo niaposema mitindo mingine iache ikupite jamani kwa maana kila mtindo una mtu wake haujaumbwa kwa wote,kuliko kuadhirika ni aiibu tupuuuuuuuuuu.yenu hiyo warembo......................................

Jan 18, 2009

CCM NA UREMBO DAM DAM?


Hilo ni swali tuu ambalo wanajiuliza baadhi ya watanzani kwa hivi sasa, kuwa bila
urembo kwenye chama au bila kupaka mapoouder haupati nafasi mjengoni?
Kuuliza swali au kutaka kujua ukweli sio kosa katika dunia yetu ya sasa,kama baadhi ya maoni na wadau wa safu hii ya kwa nafasi,wanataka kujua ukweli juu ya hili sasa sijui na wao wanataka kuingia mjengoni au nikutaka kujua tuu.
Kwanza nakitakia kila la heri chama chetu,lakini najiuliza uku tunapooenda ni wapi ?je niwakati wa urembo na madaraka?au ni wakati wa warembo kuteza na wasio warembo kusaauliwa?
kwa upande wangu mimi naona kama urembo umekuwa wakwanza katika madaraka alafu uelewa na uwezo wa mtu ni vya mwisho.hivi hapa ninapoiaandika habari hii kila mtu anakwambia unataka maisha ya starehe, jiingize kwenye chama.mmh nikashangaa ni chama hichi cha enzi hizo za akina BIBI TITI? au kingine?nikajibiwa wewe wa wapi umetoka kiboriloni nini?huna habari ya kuwa kila mtu mwenye uzuri na kujuana na watu wa chama ananafasi kubwa sana katika chama ,aaah nikashangaa sio tena uelewa ni urembo.hapo ndipo nikajijibu ndo maana kila msichana na baadhi ya viongozi ni warembo sana na baadhi yao wanamapoouder.
Sasa hapa najiuliza katika sera za elfu mbili na kumi itakuwepo sera ya urembo na na mapouder?mmh nikasema hayaaa wabaya zamu yao itafika lini? maana warembo ni wakati wao.

Jan 17, 2009

UFUNDI MWINGI MWISHO UHARIBU


Mhhh hii haijakaa vizuri kabisa na inakera watanzania wengi na wasikilizaji wa r
adio maarufu jijini bongo na mikoani.
kutokana na wapenzi wengi na wasikilizaji wa radio clouds kupenda sana kusikiliza kipindi cha POWER BREAKFAST,kilichokuwa kinaendeshwa kwa ustadi zaidi na kufanya watu wengi kukipenda hapo zamani wakati kilipokuwa kinaendeshwa na FINA MANGO NA MA
SOUD KIPANYA hivi sasa hali imekuwa kunyume kabisaaa.
Na ndo maana nikasema ufundi ukizidi huwa unaharibu,kwa matazamo wangu tuu bila kuhitaji mtu wa kujua kilikuwa kinaingiza kiasi gani? na asilimia ngapi ya watu waliokuwa wakikipenda kwa ujumla, kwa upande wote ni zaidi ya asilimia mia moja.lakini hivi sasa kipindi kimekuwa kibaya,hakifurahishi,hakina jipya ni bora kipindi.wakati huo lazima mtu ulikuwa uamke saa kumi na mbili kamili uanze kuwasikiliza na kujua kinachoendelea katika dunia.lakini hivi sasa huwa wala mtu hushtuki ukilala ukiamka ni jahazi limeanza au leo tena.sasa najiuliza hivi huwa mtu ukisifiwa sana au ukipendwa sana au ukijiona wewe ndo zaidi lazima uharibu?
Kwa hivi sasa huwa sioni wala sifikirii kipi cha kusikiliza siku za kawaida katika radio hiyo ambayo kwa sasa inaongoza kwa kusimamisha watangazaji,zaidi ya kusubiria jumapili kumsikiliza GEA HABIBU na kipindi chake cha taarabu au kusubiri michezo basi siku ipite.
Nimekaa na kutafakari hivi huwa mwaka ukiwa unaanza au mwaka ukiwa unaisha unaisha na kila kitu au ndo lazima kuwa na mabadiliko?Basi kwa mabadiliko hayo na ubunifu huo ni sawa na kupika ugali na kuufunika ukaula baada ya masaa mawili,si utakuwa umeota koti?
Wazee wa zamani wanasema siku zote huo unajifunza na yaliyopita lakini kwa radio hiyo naona NI UFUNDI MWINGI SASA WANAHARIBU.TEHETEHEEEEEEEEEEEEEE

Jan 16, 2009

soka la bongo mmh


Amakweli mtoto umleavyo ndivyo akuavyo,utajiuliza kwa nini nasema hayo sasa hvi na mie nakujibu kukumbuka shuka kukikucha ndo hali halisi ya usingizi kuanza kukutoka.
Nimekaa nikafikiri na kutazama huko tulipo toka,nikaona ngoja niweke mambo kwnye kwa nafasi,zamani wakati tunaanza kukuwa tulikuwa tunaskia radio tanzania wakitangaza sana mpira na watu walikuwa wanaenda uwanja wa taifa kwa wingi sana kiasi cha kwamba mpaka watoto wadogo walikuwa wanajua leo simba na yanga zinacheza na pia walikuwa wanajua wachezaji wa mpira utaskia wakitaniana mie ndio hamis gagarino au mie ndo gebo peter au adamu sabu na wengineo waliowika zamani.lakini hali ya sasa hvi sio kama zamani kabisa sasa sijui ni kwa nini,maana wachezaji wa mpira wa bongo hawavumi tena na wakivuma ni kwa mwaka mmoja tuu,nimefikiri nakuuliza baadhi ya watu na haya ndo majibu yao,
inajulikana wazi kwa nini wachezaji hawakai kwenye game kwa muda mrefu bwana nikauliza ni kwa nini?ETI KWA SABABU YA FITNA ZA VIONGOZ;;;;;;;;;;.hee nikabaki mdomo wazi nakujiuliza fitina na mpira wapi na wapi.sikuchoka kutafuta ukweli,mwingine akajibu WACHEZAJI MPIRA WA BONGO WANAENDEKEZA ZINAAAAAAA;;;;;.nikasema makubwa lakini hili linaukweli ndani yake.wa mwisho akanijibu usipate tabu WANAENDEKEZA BANGIIIII;;;;;;
Mhh hapo ndipo nilipogundua kuwa kwa nini soka la bongo linaenda kinyume,sasa kama kuna fitna,bangi na ngono mpira utatokea wapi,ndipo ninaoawakumbuka PAWASA,MECKY,HUSSEN MARSHA,MASATU,MUSTAFA HOZA,MWAMEJA,LUNYAMILA,sipati jibu haya mambo yamechangia wao kupotea na kusaulika kwenye soka.hhhhhha